Wednesday 27 July 2016

Ajali:Hivi ndivyo Basi la UDA lilivyogongana na Treni Kariakoo....Mmoja Afariki, 45 Wajeruhiwa

Basi la UDA lenye namba za usajili T 696 CVP limegonga treni katika eneo la Kamata Jijini Dar es Salaam usiku wa kuamkia leo  wakati Basi hilo likotokea stendi ya Gerezani Kariakoo kuelekea Mbagala na kuua mtu mmoja na wengine zaidi ya 45 kujeruhiwa.

Kaimu Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Kipolisi wa Ilala, Ernest Matiku amesema majeruhi wamepelekwa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kwa matibabu.

Hata hivyo, hakuweza kumtaja jina mtu huyo aliyefariki dunia.

“Ni kweli ajali imetokea kuna kifo cha mtu mmoja na watu wengi wameumia sana ,” amesema Kaimu kamanda huyo.

No comments:

Post a Comment