Sunday 15 October 2017

Bayern Munich yashinda ushindi mnono chini Kocha mpya Jupp Heynckes.

 
Chini ya Kocha Jupp Heynckes aliyerejea baada ya kutimuliwa kwa Carlo Ancelotti, Bayern Munich imeanza kwa kuitwanga Freiburg kwa mabao 5-0.

Katika mechi hiyo ya Bundelisga, Bayern ingeweza kushinda kwa mabao mengi zaidi.

Mabao ya Kingsley Coman, Thiago, Robert Lewandowski, Joshua Kimmich na moja la kujifunga imeifanya Bayern irejee katika mwendo wake uliozoeleka.

No comments:

Post a Comment