Matumaini ya Arsenal kutwaa taji la
ligi ya Uingereza kwa mara ya kwanza katika kipindi cha miaka 12
yalipata pigo baada yao kulazwa 2-1 na Swansea uwanjani Emirates.
Arsenal
walikuwa wakiongoza, kupitia bao la Joel Campell na ilionekana kana
kwamba wangepunguza mwanya kati yao na viongozi Leicester.Lakini Swansea, waliokuwa bila meneja wao Francesco Guidolin, walisawazisha kupitia Wayne Routledge.
Olivier Giroud na Alexis Sanchez waligonga mwamba wa goli lakini bahati haikusimama.
Ashley Williams aliwaadhibu na kufungia Swansea bao la ushindi na mwishowe Arsenal wakalazimishiwa kichapo cha 2-1.
Arsenal sasa wamo alama sita nyuma ya viongozi wa ligi Leicester City.
Tottenham, ambao walikuwa na fursa ya kwenda kileleni, nao pia waliteleza baada ya kuchezewa vilivyo na West Ham uwanjani Upton Park na kupewa kipigo cha 1-0.
Bao hilo lilifungwa kwa kichwa na Michail Antonio dakika ya saba.
Uwanjani Anfield, Liverpool walilipiza kisasi kushindwa na Manchester City kwenye Kombe la Ligi kwa kuichapa klabu hiyo ya Etihad 3-0.
Mabao ya Liverpool yalifungwa na Adam Lallana, James Milner na Roberto Firmino.
Uwanjani Old Trafford, Manchester United walikwepa msiba wa miamba wa ligi kwa kuandikisha ushindi wa 1-0 dhidi ya Watford. Bao la United lilifungwa na Juan Mata.
Matokeo kamili ya mechi zilizochezwa Jumatano usiku:
- Arsenal 1-2 Swansea
- Stoke 1-0 Newcastle
- West Ham 1-0 Tottenham
- Liverpool 3-0 Man City
- Man Utd 1-0 Watford
-
Msimamo wa ligi
P W D L GD Pts 1 Leicester City 28 16 9 3 20 57 2 Tottenham Hotspur 28 15 9 4 27 54 3 Arsenal 28 15 6 7 16 51 4 Manchester City 27 14 5 8 17 47 5 Manchester United 28 13 8 7 11 47 6 West Ham United 28 12 10 6 11 46 7 Stoke City 28 12 6 10 -3 42 8 Liverpool 27 11 8 8 5 41 9 Southampton 28 11 7 10 7 40 10 Chelsea 28 10 9 9 4 39 11 Everton 27 9 11 7 13 38 12 Watford 28 10 7 11 0 37 13 West Bromwich Albion 28 9 9 10 -7 36 14 Crystal Palace 28 9 6 13 -6 33 15 Bournemouth 28 8 8 12 -12 32 16 Swansea City 28 7 9 12 -10 30 17 Sunderland 28 6 6 16 -19 24 18 Norwich City 28 6 6 16 -22 24 19 Newcastle United 27 6 6 15 -23 24 20 Aston Villa 28 3 7 18 -29 16
No comments:
Post a Comment