Thursday 3 March 2016

Full matokeo ya michezo ya ligi ya EPL na msimamo march 2.2016

Arsenal 1-2 Swansea: Petr Cech suffers calf injury as Gunners fail to close the gap on

Matumaini ya Arsenal kutwaa taji la ligi ya Uingereza kwa mara ya kwanza katika kipindi cha miaka 12 yalipata pigo baada yao kulazwa 2-1 na Swansea uwanjani Emirates.
Arsenal walikuwa wakiongoza, kupitia bao la Joel Campell na ilionekana kana kwamba wangepunguza mwanya kati yao na viongozi Leicester.

Lakini Swansea, waliokuwa bila meneja wao Francesco Guidolin, walisawazisha kupitia Wayne Routledge.
 Arsenal's Joel Campbell slides on the ground after getting his left foot to the ball to propel past Swansea City's Lukasz Fabianski
Olivier Giroud na Alexis Sanchez waligonga mwamba wa goli lakini bahati haikusimama.
Ashley Williams aliwaadhibu na kufungia Swansea bao la ushindi na mwishowe Arsenal wakalazimishiwa kichapo cha 2-1.
Arsenal sasa wamo alama sita nyuma ya viongozi wa ligi Leicester City.
Tottenham, ambao walikuwa na fursa ya kwenda kileleni, nao pia waliteleza baada ya kuchezewa vilivyo na West Ham uwanjani Upton Park na kupewa kipigo cha 1-0.
Bao hilo lilifungwa kwa kichwa na Michail Antonio dakika ya saba.
Uwanjani Anfield, Liverpool walilipiza kisasi kushindwa na Manchester City kwenye Kombe la Ligi kwa kuichapa klabu hiyo ya Etihad 3-0.
Mabao ya Liverpool yalifungwa na Adam Lallana, James Milner na Roberto Firmino.
Uwanjani Old Trafford, Manchester United walikwepa msiba wa miamba wa ligi kwa kuandikisha ushindi wa 1-0 dhidi ya Watford. Bao la United lilifungwa na Juan Mata.
Matokeo kamili ya mechi zilizochezwa Jumatano usiku:

No comments:

Post a Comment