Duniani kuna maajabu mengi sana na wakati mwingine mengine yana shangaza na kustajabisha sana
Licha ya tofauti za kitamaduni, wanafunzi wote wana itikadi na imani zao, iwapo ni kuimba nyimbo kula chakula maalum au hata kuvaa nguo wanaoiona kuwa na bahati kwao.
Hizi ni baadhi ya mbinu zinazotumika kote Asia na wanafunzi kuhakikisha wanafualu kwa ukubwa:
- Kula tufaha kwa siku
"Tufaha kichina hutamkwa "ping guo", yaani "salama". Kwahivyo inadhaniwa utapasi mtihani salama," anasema Chong Wang, kutoka Nanjing China.
- Epuka kuosha nyele
"Kulikuwa na kijana mmoja ambaye alikuwa haoshi nyele zake kabla ya mtihani, alikuwa msafi wakati mwingine wote ila siku ya mtihani huwezi kukaribia," amesema mwanamfunzimmoja kuhusu mwenziwe darasani.
- Kula korosho
Inaaminika shughuli hizo husaidia wanafunzi kupita mitihani kwa alama za juu.
Ni muhimu kwa wanafunzi katika chakula hicho kula nyama ya ngurumwe kwa korosho.
Na chakulwa hicho hupatikana katika migahawa ya kichina ambapo Korosho kwa kichina ni neno sawa na neno"kutarajia kupasi ", na "nyama ya nguruwe" ni sawa na "hamu ya kupata alama ya juu".
- Nguvu ya kuku
Wanafunzi wa Malaysia, Hong Kong, Singapore na China hunywa supu ya kuku wanaposoma kujitayarisha kwa mitihani na asubuhi ya kuamkia mtihani wenyewe.
"Sio uchawi," anasema Dylan Lee Soon Yoong, mwanafunzi kutoka Singapore katika chuo kikuu cha London.
"Nilikunywa supu ya kuku asubuhi kuamkia mtihani ikiwa moto moto. Inatakikana kukusaidia kuwa na makini na hunywa kwa wingi na wanafunzi Singapore."
- Vaa chupi nyekundu
Kwahivyo watu wengi wanaamini ni vizuri kuvaa nguo nyekundu na zaidi chupi ya ndani wakati wa mtihani.
Wakati mtu anapofanikiwa kuna msemo wa Kichina unaosema, "umevaa chupi nyekundu?"
Lakini Chong Wang anaonya: "baadhi ya watu huepuka kuvaa ranginyekundu wakati wa mtihani kwasababu China alama za kufeli huandikwa kwa rangi nyekundu."
No comments:
Post a Comment