Friday 15 April 2016

Ratiba ya kombe la UEFA Champions Legue hii hapa

 
 Tayari ratiba ya nusu fainali ya michuano ya UEFA Champions League imeshatoka baada ya kuchezeshwa draw ya kutafuta nani ataumana na nani kati ya vilabu vinne vilivyosalia kwenye michuano hiyo baada ya Jumanne na Jumatano kushuhudia vilabu vingine vinne vikiyaaga mashindano hayo ikiwa ni pamoja na bingwa mtetezi Barcelona.


UCL2
 
Manuel Pellegrini atarejea kwenye klabu yake ya zamani baada ya Manchester City kujikuta ikitakiwa kupambana na miamba ya Hispania Real Madrid wakati Atletico Madrid watakwaana na kikosi cha Pep Guardiola Bayern Munich mechi ambazo zitapigwa April 26/27 na May 3/4.

No comments:

Post a Comment