Klabu ya soka ya Atletico Madrid
imefanikiwa kutinga fainali ya klabu bingwa barani Ulaya kwa mara ya
pili ndani ya kipindi cha miaka mitatu baada ya kupata bao la ugenini
walipokipiga dhidi ya Bayern Munchen ya Ujerumani.
Atletico wakiwa na faida ya bao la nyumbani katika nusu fainali ya kwanza nchini Uhispania, Bayern walisawazisha kupitia mkwaju wa adhabu ndogo uliopigwa na Xabi Alonso kwenye mechi ya Jumanne iliyochezewa uwanja wao wa nyumbani wa Allianz Arena.
Mlinda mlango wa Atletico Jan Oblak aliokoa mkwaju wa penalti uliopigwa na Thomas Muller kabla ya mshambuliaji Antoine Griezmann kusawazisha na kuwa 1-1.
Robert Lewandowski alifunga bao la pili baada ya kupokea pasi ya mpira wa kichwa kutoka kwa Arturo Vidal huku Atletico wakishindwa kusawazisha baada ya mkwaju wa penalti uliopigwa na Fernando Torres kuokolewa na mlinda mlango Manuel Neuer.
Matokeo ya jumla ya nusufainali hiyo yalimalizika sare 2-2 lakini Madrid wakasonga kwa kuwa na bao la ugenini.
Sasa Atletico watakutana na mshindi wa mchezo kati ya Real Madrid na Manchester City utakaopigwa kesho dimbani Santiago Bernabeu katika fainali mjini Milan tarehe 28 Mei.
|
Bayern Munich (4-1-4-1):
Neuer
6; Lahm 6, Javi Martinez 6, Boateng 6, Alaba 7; Alonso 7; Douglas Costa
6 (Coman 73min, 5), Vidal 7, Muller 6, Ribery 6; Lewandowski 7. Subs not used: Tasci, Thiago Alcantara, Rafinha, Gotze, Ulreich, Kimmich.
Booked: Javi Martinez.
Goals: Alonso 31,
Lewandowski 74
Manager: Pep Guardiola 7
Atletico Madrid (4-4-2):
Oblak
8.5; Juanfran 7, Godin 8, Gimenez 5, Filipe Luis 6; Saul Niguez 6,
Fernandez 6 (Carrasco 45, 6), Gabi 7, Koke 6 (Savic 90); Griezmann 7
(Partey 82), Torres 6. Subs not used: Moya Rumbo, Correa, Hernandez, Vietto.
Goal: Griezmann 53
Booked: Gimenez
Manager: Simeone 9
MOTM: Oblak
Referee: Cuneyt Cakir (Turkey) 7
Attendance: 70,000
Video ya Magoli
No comments:
Post a Comment