Akizungumza
Mjini Dodoma, mara baada ya kufanya ziara katika shule kongwe ya
Sekondari ya Mpwapwa, Naibu Waziri wa TAMISEMI,Mhe. Suleiman Jaffo,
amesema ameshangazwa na shule hiyo kuwa na tatizo la maji lililodumu kwa
muda mrefu kwa kukosa shilingi milioni nne.
Baada ya kushuhudia tatizo hilo Naibu Waziri huyo ametoa muda wa mwezi mmoja kwa Mkurugenzi wa Wilaya ya Mpwapwa mkoani Dodoma, kuhakikisha anatatua tatizo hilo la maji katika shule hiyo.
Mhe. Jaffo amesema kuwa ni jambo la aibu kwa taasisi kama hiyo kukosa fedha ya kutatua tatizo hilo kwa muda wa mwaka mmoja huku akitoa agizo la kufanya marekebisho ya bweni ambalo liliteketetea kwa moto na halijafanyiwa marekebisho yoyote.
Amemuagiza Mkurugenzi huyo kupita kwa wadau wa elimu kuweza kuchangia ujenzi wa baadhi ya miundombinu ya shule hiyo lakini pia wasimamie shughuli hizo ipasavyo kwa kuwa watumishi wengi wasiposimamiwa hawafanyi kazi zao
Baada ya kushuhudia tatizo hilo Naibu Waziri huyo ametoa muda wa mwezi mmoja kwa Mkurugenzi wa Wilaya ya Mpwapwa mkoani Dodoma, kuhakikisha anatatua tatizo hilo la maji katika shule hiyo.
Mhe. Jaffo amesema kuwa ni jambo la aibu kwa taasisi kama hiyo kukosa fedha ya kutatua tatizo hilo kwa muda wa mwaka mmoja huku akitoa agizo la kufanya marekebisho ya bweni ambalo liliteketetea kwa moto na halijafanyiwa marekebisho yoyote.
Amemuagiza Mkurugenzi huyo kupita kwa wadau wa elimu kuweza kuchangia ujenzi wa baadhi ya miundombinu ya shule hiyo lakini pia wasimamie shughuli hizo ipasavyo kwa kuwa watumishi wengi wasiposimamiwa hawafanyi kazi zao
No comments:
Post a Comment