Afisa
habari wa Azam FC, Jaffery Iddy Maganga, amesema mchezo uliopita dhidi
ya Simba kikosi hakikuwa kizuri kwani wachezaji walikuwa na uchovu
lakini wanaamini katika mchezo wa hapo kesho wataingia kwa nia moja ya
kupambana ili kupata pointi tatu.
Jaffery amesema, anaamini mchezo huo utakuwa mgumu kwani JKT
inapambana ili isiweze kushuka daraja kwani kwa sasa ipo katika nafasi
mbaya huku wao wakiwania kupata pointi tatu za kuwaweka katika nafasi
nzuri zaidi katika msimamo wa Ligi Kuu ya Soka Tanzania Bara.
Maganga amesema, wachezaji waliokuwa majeruhi watarudi hapo kesho kwa ajili ya kuongeza nguvu katika kikosi isipokuwa Mlinzi wao FC Pascal Wawa ambaye bado ni majeruhi lakini akiwa ameanza mazoezi madogo madogo.
Maganga amesema, wachezaji waliokuwa majeruhi watarudi hapo kesho kwa ajili ya kuongeza nguvu katika kikosi isipokuwa Mlinzi wao FC Pascal Wawa ambaye bado ni majeruhi lakini akiwa ameanza mazoezi madogo madogo.
No comments:
Post a Comment