Thursday 10 November 2016

Kauli ya mwisho ya kocha Hans van der Pluijm kwa Yanga baada ya kuondoka Rasmi Yanga.

Image result for Hans van der Pluijm
Kocha Hans van der Pluijm amesema ataikumbuka klabu ya Yanga kwa mambo mengi sana kwa kuwa ataondoka akiwa bado anaipenda.

Pluijm raia wa Uholanzi mwenye makazi yake nchini Ghana, amesema Yanga ni moja ya klabu bora kabisa alizozifundisha.

“Nitaendelea kuikumbuka Yanga kwa kuwa kwangu ni familia, nakwenda kama binadamu yoyote.

“Natoa shukurani kwa Wanayanga wote na mechi ya mwisho ya mzunguko huu wa kwanza itakuwa ya mwisho kwangu,” alisema.

Pluijm anaondika Yanga na nafasi yake inachukuliwa rasmi na kocha Geirge Lwandamina raia wa Zambia.

USISAHAU KULIKE NA KU-SHARE NA KU-LIKE PAGE YETU FACEBOOK TIKISA MEDIA KUFOLLOW TWITTER @TIKISA MEDIA NA INSTAGRAM TIKISA ENTERTAINMENT MEDIA ILI HABARI ZOTE KUBWA ZIKUFIKIE HAPO ULIPO.ASANTE

                              SUBSCRIBE ON YOUTUBE TIKISA TV

No comments:

Post a Comment