Tuesday 6 December 2016

Serikali ya Tanzania kuongeza adhabu kwa wanaojiusisha na Rushwa.

Image result for Angellah Kairuki ikulu
Serikali imeeleza dhamira yake ya kuongeza adhabu kwa watu wanaobainika kuhusika na rushwa ili wawe wanalipa fidia ya hasara iliyojitokeza mbali na kutumikia kifungo.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Utumishi na Utawala Bora Mh. Angellah Kairuki amesema kuwa adhabu zinazotolewa kwa wala rushwa ni ndogo ikilinganishwa na hasara wanayoisababishia serikali, hivyo marekebisho ya sheria hizo itamtaka mlarushwa kulipa fidia ya hasara iliyojitokeza

Akiongea na waandishi wa habari, mara baada ya kuzinduliwa kwa wiki ya kupokea malalamiko ya wananchi, katika viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam, Mhe Angella amesema serikali itahakiki mali za viongozi wa serikali wapatao 500 na kuwataka wananchi kujitokeza kuhakiki mali za viongozi wao pamoja na kutoa taarifa ambazo serikali haikufanikiwa kuzipata.

USISAHAU KULIKE NA KU-SHARE NA KU-LIKE PAGE YETU FACEBOOK TIKISA MEDIA KUFOLLOW TWITTER @TIKISA MEDIA NA INSTAGRAM TIKISA ENTERTAINMENT MEDIA ILI HABARI ZOTE KUBWA ZIKUFIKIE HAPO ULIPO.ASANTE



                                SUBSCRIBE ON YOUTUBE 
                                          
                                               TIKISA TV

No comments:

Post a Comment