Monday 30 January 2017

Donald Trump atoa ufafanuzi kuhusu sera ya uamiaji nchini Marekani.

Rais wa Marekani Donald Trump ametetea marufuku yake ya muda ya kusafiri kwa watu wanaotoka katika nchi saba ambazo ni za kiislamu baada ya watu kuukosoa uamuzi huo huku wengine wakiandamana.

Katika taarifa ya maandishi, bwana Trump amevilaumu vyombo vya habari kwa kupotosha taarifa kwamba marufuku hiyo ni kwa waislamu.
Amesema viza zitatolewa kwa wasafiri kutoka nchi zote ndani ya siku tisini.

Katika hali inayoonekana kulegeza msimamo wa amri ya kiutendaji iliyopitishwa siku ya Ijumaa, Reince Priebus, ambae ni kiongozi wa wafanyakazi wa serikali amesema marufuku hiyo haitawahusu wenye kuhodhi kadi za green, ambao wana haki ya kisheria kuishi nchini Marekani.
Mhariri wa BBC kaskazini mwa marekani amesema ikulu ya marekani imekosolewa vikali kwa sera hiyo.
Wakati huo huo, maelfu ya waandamanaji wanaopinga amri hiyo ya Trump kwa mara nyengine wameandamana katika viwanja vya ndege na sehemu nyinginezo nchini Marekani.
Mamia ya watu wameandamana kupinga hatua hiyo
Mamia ya watu wameandamana kupinga hatua hiyo
Waandamanaji wamepita katika miji ya Boston, New York na karibu na ikulu mjini Washington.
A huge crowd of people is seen in Boston's Copley Square on Sunday during protests against the new immigration policy put forward by Trump this week
Waandamanaji wanaopinga sera hiyo ya Trump.
Mwanasiasa mwandamizi wa Republican ambae pia ni mwenyekiti wa kamati ya senate ya mambo ya nje, Bob Corker, amesema amri hiyo ya Rais utekelezaji wake haukuwa na ufanisi,hivyo kutaka mabadiliko ya haraka kufanywa.
Washauri wakuu wa masuala ya sheria kutoka majimbo kumi na sita nchini Marekani wameshutumu marufuku hiyo ya kusafiri na kusema haiko kisheria, imekiuka maadili ya kimarekani na imekiuka katiba ya nchi.
Kwa upande wake, Hakeem Jeffries kutoka chama cha Demokrat, alikuwa ni miongoni mwa walioandamana katika uwanja wa ndege wa JFK mjini New York.
Amesema idadi kubwa ya watu wanazuiwa kinyume cha sheria katika uwanja wa ndege.

No comments:

Post a Comment