Akizungumza katika Mkutano wa hadhara Bw. Gambo amesema ni vyema migogoro hiyo inapojitokeza ikatatulia kwa njia ya mashauriano kwa pande zinazo kinzana badala ya wananchi kujichukulia sheria mikononi ya kuvamia mashamba hayo.
"Ni kosa kwa wananchi kuvamia mashamba ambayo yana hati miliki halali, serikali ya haitavumilia kuona vitendo hivyo vikiendelea tutachukua hatua kwa wale wote watakaobainika kufanya uvamizi huo", amesema Gambo.
Kwa upande wake Mkurugenzi wa Halmshauri ya Meru, Christpher Kazeri amesema wamekua wakiifanyia kazi migogoro hiyo huku afisa mipango miji wa Halmashauri hiyo Shahidi Chuma, ameahidi kutafuta suluhu ya migogoro hiyo baina ya kijiji cha Magadini na maloloni.
No comments:
Post a Comment