Monday 14 August 2017

Kama wewe ni kijana Fursa hii isikupite kutoka serikalini.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Uratibu na Bunge, Mhe Jenista Mhagama amefunguka na kusema serikali ya awamu ya tano imeweka mpango kila wilaya kutenga maeneo ya vijana kuanzisha kilimo cha 'Green house'

Aidha Waziri Jenista Mhagama amewataka vijana kila sehemu kwenda kwenye ofisi za Wakuu wa Wilaya na Wakuu wa Mikoa ili waweze kuwaeleza ni kwa kiasi gani wameanza kuratibu mpango huo wa kuwa na kilimo cha kisasa kwa kila wilaya na kila mkoa kwa vijana.  

No comments:

Post a Comment