Wednesday 23 August 2017

Record aliyoiacha Wayne Rooney baada ya kustaafu katika Timu yake ya Taifa.

Wayne Rooney has called time on his England career by announcing  international retirement
Mfungaji wa mabao mengi nchini Uingereza Wayne Rooney ameamua kustaafu katika soka ya kimataifa baada ya kukataa kushirikishwa katika kikosi cha timu ya taifa ya Uingereza kitakachomenyana katika mechi za kufuzu kombe la dunia.

Mshambuliaji huyo wa Everton aliombwa na meneja wa timu ya kandanda ya Uingereza kushiriki katika mechi dhidi ya Malta na Slovakia.
Gareth Southgate wanted to recall him to the squad for the  games against Malta and Slovakia
''Kila mara nilipochaguliwa ilikuwa fahari kubwa kwangu lakini naamini imefikia muda wa kujiondoa'' , alisema mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 31.
Mshambuliaji huyo wa zamani wa Manchester United alifunga mabao 53 katika mechi 119 za kimataifa.
Rooney pictured on his debut against Australia in 2003
Rooney ambaye hakushirikishwa na Southgate katika mechi dhidi ya Scotland na Ufaransa mnamo mwezi Juni alianza kuichezea Uingereza mwaka 2003 katika mechi ambapo Uingereza ilipoteza kwa Australia.
orodha ya wafungaji vinara.
1.Wayne Rooney 53
2.Bobby Charlton 49
3.Gary Lineker 48
4.Jimmy Greaves 44
5.Michael Owen 40
6.Tom Finney 30
7.Nat Lofthouse 30
8.Alan Shearer 30
9.Viv Woodward 29
10.Frank Lampard 29 

No comments:

Post a Comment