"Mungu Baba uliyeahidi kuipenda Tanzania na Watoto wako, timiza Upendo wako. Mjalie Kaka yetu Lissu afya na uzima.amina" aliandika Mbunge Ridhiwani Kikwete
Watanzania wengi wameonyesha kuguswa na kulaani kitendo hicho alichofanyiwa mbunge huyo huku wengi wao wakimuombea aweze kupata afya njema na kupona, kwa upande wa Zitto Kabwe amewataka watanzania kila mmoja kwa imani yake kumuombea kiongozi huyo ili aweze kupona.
"Tumwombee Tundu Lissu. Kila mtu aombe kwa imani yake. Mungu ampe nafuu Inshallah" Aliandika Zitto Kabwe
"Nimepokea kwa masikitiko tukio la kupigwa risasi Mh.Tundu Lissu, namuombea kwa Mwenyezi Mungu aweze kupona haraka. Vyombo vya dola viwasake wale wote waliohusika na tukio hilo la kinyama na kuwafikisha katika mikono ya sheria", ameandika Rais Magufuli.
No comments:
Post a Comment