Tuesday, 19 September 2017

Cannavaro aibua mapya baada ya kuonana na Yusuf Manji.


Suala la nahodha wa Yanga, Nadir Haroub Ally maarufu kama Cannavaro kukutana na Mwenyekiti wa zamani wa Yanga, Yusuf Manji limezua mjadala mkubwa.

Katika mitandao mbalimbali, suala hilo limekuwa likijadiliwa na kila mtu akiamini kivyake.

Wako wamekuwa wakiamini Cannavaro ambaye aliongozana na benchi la ufundi, walikwenda kumjulia hali Manji katika mahakama ya Kisutu.

Wako wamekuwa wakiamini walikwenda kumlilia shida kwa kuwa mambo yao si mazuri na kadhalika.

Mjadala huo sasa umekuwa ukiendelea kwa takribani saa 24 katika mitandao hiyo ya kijamii.

No comments:

Post a Comment