Tuesday, 12 September 2017

Hivi ndio Vikwazo vipya walivyowekewa Korea Kaskazini.

Image result for Kim Jong Un
Rais wa korea Kaskazini Kim Jong Un
Baraza la usalama la umoja wa mataifa limepiga kura kwa kauli moja kuiwekea vikwazo Korea Kaskazini kama adhabu ya kufanyia majaribio zana zake za nuklia.

Vikwazo hivyo vinalenga kuhujumu uwezo wa Pyongyang kufadhili na kutoa kawi kwa mpango wake wa nuklya.
Vikwazo hivyo vile vile vinatoa masharti kwa biashara ya kununua mafuta ya Korea Kaskazini mbali na kupiga marufuku uuzaji wa nguo katika mataifa ya kigeni.
Maamuzi hayo ya baraza la usalama la umoja wa mataifa yaliungwa mkono kwa wingi wa kura baada ya Marekani kuondoa mpango wake wa kutaka uungwaji mkono kutoka Urusi na China
Korea Kusini inasema kuwa kwa kuhujumu amani Korea Kaskazini itaewekewa vikwazo zaidi vya kimataifa.
Balozi wa China katika Umoja wa kimataifa Liu Jieyi ameitaka Korea kaskazini kuchukua kwa muhimu mkubwa matarajio ya ya jamii ya kimataifa na kuharibu mpango wao.

No comments:

Post a Comment