Friday 29 September 2017

Matokeo ya mechi zote za Michuano ya Uefa Europa Ligi.

Michuano ya Uefa Europa Ligi imepigwa usiku wa kuamkia leo kwa michezo mbalimbali hatua ya Makundi.


Klabu ya Arsenal ikiwa ugenini Imeshinda mabao 4-2 dhidi ya Bate Borisov, Everton imetoka sare ya bao 2-2 na Apollon, Ac Millan imeshinda 3-2 dhidi ya Rijea, Lyon pia wamefanikiwa kutoa sare na Atlanta baada ya kufungana bao 1-1.
Nice imeichapa Vitese mabao 3-0, Mainz imefungwa bao 1-0 na Hoffeinheim, Partizan imechapwa na Dynamo magoli 3-2 na Maccab Tel Aviv imetoka sare na Villareal 0-0.
Fc sheriff imetoshana nguvu na Koeben kwa sare ya kutofungana 0-0, Lugan imeambulia kipigo cha bao 2-1 dhidi ya FC FCSB ,Plesen imeichakaza Hapoel bao 3-0.
FC Cologne imefungwa bao 1-0 na FK Crvena Zvezda, Salzburg imeshinda bao 1-0 dhidi ya Marseille, Oestersunds FK imeichapa Hertha Berlin bao 1-0, Konyaspor imetakata kwa ushindi wa bao 2-1 na Vitoria de Guimaraes.
AEK Athens imetoshana nguvu na Austria Wien ya bao kwa kufungana bao 2-2.


No comments:

Post a Comment