Wednesday 28 February 2018

Asante Kwasi afichua siri ya kilichompeleka upande wa benchi la ufundi Mbao FC.

Image result for asante kwasi
Katika mchezo uliochezwa Jumatatu dhidi ya Mbao, Kwasi alikwenda katika benchi la Mbao zaidi ya mara tatu kusikiliza maagizo waliyopewa wachezaji kisha kwenda kuwaambia wenzie kinachojiri.

Kwasi alisema kuwa, kitendo alichokuwa akikifanya ni mbinu ya kiuanamichezo kuweza kuwamaliza wapinzani wao kwa lengo la kufahamu maelekezo wanayopewa ili kuyafanyia kazi.

“Tumefurahi matokeo haya ya ushindi wa mabao matano, lengo letu ni kuona tunafanikiwa kufanya vizuri kila mechi tunayocheza ili kufanikiwa kutwaa ubingwa mwishoni mwa msimu.

“Mara nyingi nimekuwa nikienda kwa benchi la wapinzani kusikiliza, hii ni moja ya mbinu ya kimchezo  ambayo inasaidia kuwasoma wapinzani wetu na kujua wanataka kufanya nini ili kuweza kujihami, ni mbinu ya kawaida ambayo inafanywa sehemu yoyote,” alisema Kwasi.



 Aidha beki huyo, ana mabao sita hadi sasa aliyoyafunga kwenye ligi huku akiwa amefunga akiwa Lipuli FC matano na moja akiwa  na Simba.

No comments:

Post a Comment