Friday 23 October 2015

MAAMUZI YA UEFA KUHUSU MASHABIKI WA TIMU DYNAMO KIEV HAYA HAPA



Shirikisho la Soka barani Ulaya Uefa, limefungua kesi ya kinidhamu dhidi ya klabu ya Dynamo Kiev kutokana na vurugu zilizofanywa na mashabiki wake na mambo ya kibaguzi katika mchezo wa Ligi ya mabingwa Ulaya dhidi ya Chelsea. Katika taarifa yake Uefa imesema itaanza kusikiliza kesi hiyo Octoba 27 mwaka huu. Hiyo sio mara ya kwanza kwa mashabiki wa timu hiyo kuingia matatani kwani katika msimu uliopita Dynamo walitozwa faini ya kufungiwa upande mmoja wa uwanja kwa makosa mawili mojawapo likiwa vurugu na lingine ubaguzi katika mchezo wa michuano ya Europa League.
                                         Eden Hazard akiwatoka wachezezaji wa Dynmo
                                   Kocha wa chelsea (kulia) Jose Mourinho na Eden Hazard

No comments:

Post a Comment