Monday 21 December 2015

CHAMA cha Mapinduzi mkoani Lindi kimetetea jimbo lake la Masasi katika uchaguzi ulifanyika Jana baada ya kuahirishwa Oktoba 25 Mwaka



 
CHAMA cha Mapinduzi mkoani Lindi kimetetea jimbo lake la Masasi katika uchaguzi ulifanyika Jana baada ya kuahirishwa Oktoba 25 Mwaka huu kutokana na kifo cha aliyekuwa Mgombea ubunge wa Jimbo hilo kupitia Chama Cha NLD, Dokta Emamanuel Makaidi kufariki Dunia
Kwa mujibu wa matokeo ya uchaguzi huo yaliyotangazwa na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jimbo la Masasi, Fortunatus Kagoro amesema kuwa Bwana Rashid Chuachua amepata kura 16,597 akifuatiwa na Ismail Makombe Maarufu kama Kundambanda wa CUF, aliyepata kura 14,019.
Wengine Walioshiriki katika Uchaguzi huo ni Swaleh Ahmad wa CHADEMA, aliyepata kura 512, Omary Timothy wa ACT-Wazalendo Aliyepata kura 347, na Angelus Thomas wa NLD Aliyepata kura 70.

No comments:

Post a Comment