Monday 21 December 2015

KATIBU tawala wa mkoa wa Shinyanga, Abdul Dachi, ameziagiza Halmashauri zote sita za mkoani humo kutenga bajeti ya lishe ya katika mwaka wa fedha 2016/17











KATIBU tawala wa mkoa wa Shinyanga, Abdul Dachi, ameziagiza Halmashauri zote sita za mkoani humo kutenga bajeti ya lishe ya kkatika mwaka wa fedha 2016/17 kwa lengo la kuondoa tatizo la utapiamlo kwa watoto
Takwimu zinaonyesha mkoa huo ni miongoni mwa mikoa nchini, inayokabiliwa na asilimia kubwa ya watoto wenye utapiamlo na udumavu na kusababisha kuzalisha kizazi cha watu wenye afya mgogoro na kushindwa kujenga taifa lao.
Dachi ametoa agizo hilo wakati akifungua kikao cha wadau wa afya mkoani Shinyanga, kilichoandaliwa na shirika la Save the children kwa madhumuni ya kutoa taarifa ya mradi wa ANI na kupanga mikakati mipya ya kutokomeza tatizo la utapiamlo kwa watoto
Naye afisa lishe mkoa, Mariamu Mwita, amesema takwimu za utapiamlo mkoani humo ni asilimia 43 kwa watoto wadumavu, 75 wakiwa na upungufu wa samu, madini chuma asilimia 48, vitamin A 37, waliokonda 3 na uzito pungufu 10.
Kwa upande wake afisa mradi wa kupambana na utapiamlo mkoani Shinyanga toka shirika hilo, Augustino Mwashiga, amesema mradi huo wa Accelerating nutrion improvement Ani, umefanyika kwa miaka miwili 2014/15 uliokuwa na lengo la kuhamasisha jamii kufuata sheria za lishe bora.

No comments:

Post a Comment