Tuesday 29 December 2015

KLABU ya Arsenal imeanza mazungumzo na FC Basel ya Uswisi kwa ajili ya kutaka kumsajili kiungo wao Mohamed Elneny.

KLABU ya Arsenal imeanza mazungumzo na FC Basel ya Uswisi kwa ajili ya kutaka kumsajili kiungo wao Mohamed Elneny. 
Nyota huyo wa kimataifa wa Misri mwenye umri wa miaka 23 alijiunga na klabu hiyo mwaka 2013 na kufanikiwa kushinda mataji ya Ligi Kuu ya nchi hiyo kwa misimu mitatu
 
 Elneny anakadiriwa kuwa na thamani ya paundi milioni tano, ingawa atahitaji kibali cha kufanyia kazi nchini Uingereza. Kama Arsenal wakifanikiwa kumsajili wanaweza kumtumia katika michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya kwani Basel
 
       Mohamed Elneny

Hawakufanikiwa kufuzu hatua ya makundi msimu huu. 
Meneja wa Arsenal Arsene Wenger anajaribu kuongeza nguvu safu yake ya kiungo baada ya Francis Coquelin na Santi Cazorla kupata majeruhi ya muda mrefu huku Aaron Ramsey na Mikel Arteta nao wakikosa michezo kadhaa kutokana na majeruhi.

No comments:

Post a Comment