Monday 28 December 2015

MTU mmoja amefariki dunia na wengine wanne kujeruhiwa baada ya gari moja linalosadikiwa kubeba mabomu kuripuka karibu na uwanja wa ndege wa kimataiafa mjini Qaboul-Afghanistan



 
MTU mmoja amefariki dunia  na  wengine  wanne kujeruhiwa baada ya  gari moja linalosadikiwa kubeba mabomu kuripuka karibu na uwanja wa ndege wa kimataiafa mjini Qaboul-Afghanistan  mapema leo.  
Duru za ki usalama  za nchi hiyo zinaripoti kuwa  gari hilo lilikuwa limelenga  gari la vikosi  vya  umoja wa kujihami wa nchi za magharibi NATO
Tukio hilo limekuja sambamba na ujio wa  Amiri jeshi mkuu wa Pakistan generali Raheel sharif kuwasili nchini Afghanistan ili kufanya mazungumzo ya amani  na  viongozi wan chi hiyo.
Tukio hilo ni la pili  kutokea  ambapo  mwezi uliopita jeshi la Afghanistan liliripoti kuwa watu  37 walipoteza maisha  yao  na wengine kadhaa kujeruhiwa katika hujuma iliyopangwa na kundi la Taliban   katika uwanja wa ndege wa kandahari

No comments:

Post a Comment