WAZIRI wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Mafunzo
ya Ufundi, Prof. Joyce Ndalichako, amesema atafuatilia shule za Serikali ili
kujua sababu za kufanya vibaya katika mitihani yao. Prof. Ndalichako ambaye
aliwahi kuwa Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani (NECTA),
“Kwa kuwa lengo langu ni kuona elimu bora
inatolewa, nitafuatilia kujua sababu ya shule maalumu za Serikali kushuka
kiwango chake katika ufaulu wa mitihani,”
Kwa mujibu wa Prof. Ndalichako, shule hizo za
Serikali hasa za vipaji maalum, ndizo awali kila mwanafunzi alipenda kwenda
kusoma tofauti na sasa ndio maana anataka kujua kulikoni.
Shule hizo ni pamoja na Mzumbe, Ilboru, Tabora
Wavulana, Tabora Wasichana, Kilakala na Msalato.
Ada holela, kukaa chini
Kuhusu upandaji holela wa ada za shule binafsi,
Prof. Ndalichako alisema atapambana na vyuo vikuu na shule binafsi, zinazofanya
ujanjaujanja wa kupandisha ada tofauti na ile iliyoandikwa kwenye barua za
kuwaita wanafunzi, jambo linalosababisha usumbufu kwa wazazi.
Alisema lengo lake ni kuhakikisha Tanzania inatoa
elimu bora kwa wahitimu wa vyuoni na sekondari, itakayowawezesha kukidhi soko
la ajira la kimataifa. Pamoja na ubora huo, Prof. Ndalichako alisema ataangalia
uwepo wa miundombinu kwa wanafunzi wa kuanzia shule ya msingi na sekondari,
ambako alikiri kuwa baadhi ya wanafunzi wanaketi chini na wengine wana matatizo
ya mashimo ya vyoo.
“Inakuwaje shule yenye maelfu ya wanafunzi
watumie shimo moja la choo, haya na mambo mengine yanakwaza wanafunzi wasipende
shule na wengine wakatize masomo yao.
“Tunataka kuandaa mwanasayansi, hivi kweli mwanafunzi anayeketi chini anaweza kuwa mtaalamu mzuri wa sayansi? Ni lazima tuwezeshe shule zetu ziwe na miundombinu rafiki kwa wanafunzi”
“Tunataka kuandaa mwanasayansi, hivi kweli mwanafunzi anayeketi chini anaweza kuwa mtaalamu mzuri wa sayansi? Ni lazima tuwezeshe shule zetu ziwe na miundombinu rafiki kwa wanafunzi”
Pia alisema atashughulika na tatizo la baadhi ya
vyuo kutoa kozi zinazoenda kinyume na ithibati walizopewa na mamlaka za elimu,
jambo linalofanya wanafunzi wanaosoma kwenye vyuo hivyo kutotambuliwa na
waajiri.
No comments:
Post a Comment