Thursday 28 April 2016

Mashindano ya kimataifa ya Riadha kuanza kesho jijini Dar es salaam.

Mashindano ya kimataifa ya Riadha ya kikanda ya vijana chini ya miaka 20 yanatarajiwa kuanza kutimua vumbi hapo kesho Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam.
Makamu wa kwanza wa Rais wa Chama cha Riadha Tanzania RT Wiliam Kalage amesema, nchi shiriki 11 za michuano hiyo zimeshawasili pamoja na viongozi zikiwa tayari kwa ajili ya mashindano hayo yatakayofikia tamati Aprili 30 mwaka huu siku ya jumamosi.

Kalage amesema, timu zote shiriki zimefikia eneo maalumu ambalo ni kijiji cha michezo kilicho andaliwa kwa ajili ya mashindano hayo huku ratiba rasmi ya ufunguzi wa mashindano hayo ikitarajiwa kutatolewa hapo kesho mchana.

Nchi shiriki za mashindano hayo ni Kenya, Uganda, Rwanda, Elitrea, Sudan, Ethiopia, Sudan Kusini, Zanzibar, Djibout na Tanzania ambaye ni mwenyeji wa mashindano hayo

No comments:

Post a Comment