Thursday 21 April 2016

Mwili wa Brig.Jenerali Mstaafu Ernest Galinoma kuzikwa leo mkoani Iringa(+picha)

Mkuu wa wilaya ya Iringa Mh Richard Kasesela ( kushoto ) akiwa na makamanda wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania ( JWTZ ) katika mapokezi ya mwili wa Brig General (Mstaafu) Ernest Galinoma nyumbani kwake Kalenga. 
Jana tarehe 20/04/2016 usiku Mkuu wa wilaya ya Iringa Mh Richard Kasesela aliongoza waombolezi katika mapokezi ya mwili wa Brig General (Mstaafu) Ernest Galinoma nyumbani kwake Kalenga. 

Marehemu alifariki juzi jijini Dar es Salaam na anatarajiwa kuzikwa leo katika makaburi ya Kalenga.

Shughuli za ibada zitaanza saa 6 mchana katika kanisa katoliki Kalenga. Bwana ametoa Bwana ametwaa jina la Bwana lihimidiwe.
Makamanda wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania ( JWTZ ) wakiteremsha mwili wa Brig General (Mstaafu) Ernest Galinoma baada ya kuwasili nyumbani kwake Kalenga.
Makamanda wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania ( JWTZ ) wakiwa wamebeba jeneza lenye  mwili wa Brig General (Mstaafu) Ernest Galinoma kuuingiza nyumbani kwake Kalenga.

No comments:

Post a Comment