Friday 15 April 2016

NMB kudhamini kampuni za watoa huduma za afya

Benki ya NMB imesaini mkataba wa makubaliano na taasisi ya kutoa mikopo kwa huduma za afya ya Uholanzi - MCF ili kudhamini kampuni ndogo za watoa huduma za afya, hospitali na maduka ya dawa binafsi kujipatia mikopo ya kati ya shilingi milioni 30 na bilioni mbili.
Afisa Mtendaji Mkuu wa Medical Credit Fund (MCF)- Bi Monique Dolfing-Vogelenzang (kushoto) na Mkurungenzi Mtendaji wa NMB - Bi Ineke Bussemaker wakisaini makubaliano yatakayowezesha sekta ya afya kupata mikopo nafuu kutoka NMB
Benki ya NMB imesaini mkataba wa makubaliano na taasisi ya kutoa mikopo kwa huduma za afya ya Uholanzi - MCF ili kudhamini kampuni ndogo za watoa huduma za afya, hospitali na maduka ya dawa binafsi kujipatia mikopo ya kati ya shilingi milioni 30 na bilioni mbili.
Wakizungumza wakati wa utilianaji saini mkataba huo Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NMB, INEKE BUSSEMAKER na Afisa Mtendaji Mkuu wa MCF, MONIQUE DOLFING-VOGELENZANG wamesema ushirikiano huo umekuja wakati muafaka ambapo utaongeza utoaji wa huduma za kiafya katika maeneo mengi.
Naye Afisa wa huduma za kibenki kwa wateja wadogo wa NMB ABDULMAJID NSEKELA amesema mikopo hiyo itawalenga zaidi wamiliki wa hospitali na maduka ya dawa binafsi ambao wanahitaji mitaji ya kukuza biashara zao.

No comments:

Post a Comment