Akitoa maagizo hayo mbele ya Kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa Dkt. KEBWE amesema amefikia uamuzi huo baada ya kubaini kuwa kiwanda hicho kilikuwa kimefungiwa na serikali tangu mwaka 2010 lakini kikakiuka agizo hilo na kuendelea na uzalishaji huku maafisa hao wa Halmashauri wakishindwa kufuatilia mapato ya Halmashauri kwa kipindi cha miaka sita mfululizo.
Waliokamatwa kujihusisha kuendesha mgodi huo kinyume cha sheria ni pamoja na SHIQING LIANG ,WANG JUN na HILARY PAUL wote wakiwa ni wafanya kazi wa mgodi huo.
Dkt. Kebwe pia ametembelea baadhi ya maeneo ya mgodi huo na kubaini shughuli nyingine za usafishaji wa dhahabu kinyume cha taratibu ambapo pia amekuta viroba vilivyofungashwa mchanga wa dhahabu.
No comments:
Post a Comment