Waziri
wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi WILLIAM LUKUVI amepiga marufuku
benki zote nchini kutoa mikopo kwa kutumia dhamana ya viwanja vyenye
ofa
Waziri LUKUVI ametoa kauli hiyo jijini DAR ES SALAAM alipokutana na kufanya mazungumzo na jumuiya ya wenye mabenki nchini kujadili jinsi watakavyochangia kuongeza kasi ya watanzania kupimiwa viwanja na utatuzi wa changamoto mbalimbali zilizo kwenye sekta ya ukopeshaji kupitia ardhi.
Halikadhalika Waziri LUKUVI amezitaka benki kuhakikisha zinakua na mfumo wa ufuatiliaji wateja wanaokopa fedha kwa ajili ya miradi ya kilimo ili kujiridhisha kama fedha hizo zimetumika kama zilivyoombwa ama vinginevyo.
No comments:
Post a Comment