Rais
wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania Dk. John Pombe Magufuli ambaye pia
ni Mwenyekiti wa Jumuiya ya Afrika Mashariki CEAC) na Rais wa Jamhuri ya
Sudan Kusini Mhe. Salva Kiir wakibadilishana hati za makubaliano ya
kujiunga na Jumuiya ya Afrika Mashariki mara baada ya kusaini
Mwezi uliopita, viongozi wa nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki waliidhinisha kukubaliwa kwa SUDAN KUSINI kujiunga na jumuiya hiyo kwenye mkutano wa wakuu wa nchi hizo zinaounda Jumuiya hiyo uliofanyika mjini ARUSHA.
SUDAN KUSINI inakuwa nchi ya SITA kujiunga na Jumuiya ya Afrika Mashariki.
Baada ya kujiunga rasmi leo, SUDAN KUSINI inatarajiwa kufungua mipaka yake kwa ajili ya biashara.
No comments:
Post a Comment