Jaji
Mkuu ameyasema hayo alipokuwa akihutubia wadau wa vyombo vya habari
ambao wamekusanyika jijini Mwanza katika kuadhimisha siku ya uhuru wa
vyombo vya habari duniani ambapo kauli mbiu mwaka huu inasema kupata
habari ni haki yako idai.
Jaji mkuu amesisitiza kuwa vyombo vya habari viliweza kufanya kazi kubwa ya kuwaelimisha wananchi na pia kutoa habari kuhusiana na mwenendo mzima wa uchaguzi jambo ambalo lilifanya wananchi kuweza kushiriki kikamilifu.
Aidha ameongeza kuwa kukua kwa teknolojia ya 'internet' nchini kumechangia wasomaji wa magazeti kupungua kutokana na wananchi kupata taarifa kupitia mitandao ya kijamii ila bado changamoto hiyo siyo kubwa sana.
Mei 03 ya kila mwaka dunia huadhimisha siku ya vyombo vya habari ambapo wadau wa vyombo vya habari hushiriki katika makongamano maalum, katika kujadili mambo yanayokwamisha uhuru wa vyombo vya habari pamoja na namna ya kusonga mbele kiutendaji.
Maadhimisho kwa upande wa Tanzania yanafikia kilele leo ambapo wadau wa habari zadi ya 250 wameungana mkoani Mwanza ambapo Waziri wa Habari Nape Nnauye na Mwenyekiti wa Vyombo vya Habari Dkt. Regnald Mengi ni miongoni mwa wageni walioalikwa.
Jaji mkuu amesisitiza kuwa vyombo vya habari viliweza kufanya kazi kubwa ya kuwaelimisha wananchi na pia kutoa habari kuhusiana na mwenendo mzima wa uchaguzi jambo ambalo lilifanya wananchi kuweza kushiriki kikamilifu.
Aidha ameongeza kuwa kukua kwa teknolojia ya 'internet' nchini kumechangia wasomaji wa magazeti kupungua kutokana na wananchi kupata taarifa kupitia mitandao ya kijamii ila bado changamoto hiyo siyo kubwa sana.
Mei 03 ya kila mwaka dunia huadhimisha siku ya vyombo vya habari ambapo wadau wa vyombo vya habari hushiriki katika makongamano maalum, katika kujadili mambo yanayokwamisha uhuru wa vyombo vya habari pamoja na namna ya kusonga mbele kiutendaji.
Maadhimisho kwa upande wa Tanzania yanafikia kilele leo ambapo wadau wa habari zadi ya 250 wameungana mkoani Mwanza ambapo Waziri wa Habari Nape Nnauye na Mwenyekiti wa Vyombo vya Habari Dkt. Regnald Mengi ni miongoni mwa wageni walioalikwa.
No comments:
Post a Comment