Naibu Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Injinia Edwin
Ngonyani amesema kwamba serikali ya awamu ya tano ikisema jambo
inamaanisha na ikiahidi inatenda kama ilivyo ahidi hivyo wananchi
waiamini.
Ngonyani
ameyasema hayo Bungeni alipokuwa akijibu swali la Mbunge Juma Nkamia
(CCM) kuhusu kipande cha barabara kutoka chuo cha Mipango Dodoma kwenda
Msalato kiasi cha kilomota 8 na zaidi ziliahidiwa kujengwa kwa lami na
hadi sasa bado hazijafanyiwa kazi.
Akijibu swali hilo Naibu waziri wa Ujenzi Ngonyani amesema serikali
hii ikiahidi inatenda na kwamba barabara hilo tayari mkandarasi
atawasili katika eneo la kazi baada ya kulipwa stahiki zake.
Aidha serikali imeitaka TANROADS kuanza kukarabati barabara
mbalimbali nchini ambazo zimeharibika kufuatia mvua za masika kunyesha
No comments:
Post a Comment