Klabu ya soka ya Leicester City
wameshinda taji la ligi kuu England katika historia inayovutia kwenye
ligi hiyo. Suluhu ya 2-2 waliyoipata Tottenham dhidi ya Chelsea siku ya
jumatatu usiku ilisababisha mafanikio hayo makubwa kuwahi kutokea kwa
upande wa Claudio Ranieri.
Lakini wamepoteza michezo mitatu tu katika kile kinachotafsiriwa kama hadithi za kale na ushindi wa kipekee katika timu hiyo. Wapinzani wao wa karibu Spurs,Arsenal,Manchester City, Manchester United na washindi wa ligi msimu uliopita Chelsea wameshindwa kuwazuia mbweha katika msimu mzima wa ligi.
''Kwa kigezo cha soka la ndani,Leicester City kushinda taji la ligi kuu ni mafanikio makubwa sana katika historia na haiwezi kusahaulika'' kiungo wa zamani wa Leicester Robbie Savage ameiambia BBC.''Ni jambo la ajabu.Hii ni hatua ya mageuzi katika historia ya Ligi Kuu."
Rais wa shirikisho la soka duniani Gianni Infantino amesema historia nzuri ya Leicester ilikua ni kama hadithi za kale.
Harry Kane alichoandika katika ukurasa wake wa Twitter
Jamie vardy
No comments:
Post a Comment