Saturday 11 June 2016

Breaking News:Huu ndio uteuzi Rais John Pombe Magufuli alioufanya leo tarehe 11 June 2016.

magu
Rais John Pombe Magufuli leo tarehe 11 June 2016, amemteua Mhe. Mwigulu Lameck Nchemba kuwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya nchi. Mhe. Nchemba anachukua nafasi iliyoachwa wazi na aliyekuwa Waziri wa wizara hiyo, Mhe. Charles Muhangwa Kitwanga ambaye uteuzi wake ulitenguliwa.


Wakati huo huo rais amemteua mbunge wa Buchosha Dkt. Charles John Tizeba kuwa Waziri wa Kilimo, Mifugo na uvuvi, nafasi iliyokua ikishikiliwa na Mhe. Nchemba.
 
Wateuliwa wataapishwa siku ya Juma tatu majira ya saa 3:00 asubuhi Ikulu.



USISAHAU KULIKE NA KUSHARE PAGE YETU FACEBOOK TIKISA MEDIA KUTU FOLLOW TWITTER @TIKISA MEDIA NA INSTAGRAM TIKISA ENTERTAINMENT MEDIA ILI HABARI ZOTE KUBWA ZIKUFIKIE HAPA ULIPO.ASANTE

No comments:

Post a Comment