Monday 18 July 2016

Haya ndio majibu kutoka IKULU kuhusu Rais Magufuli kumteua Jerry Muro kuwa Msaidizi wa Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu.

Kuna ujumbe umesambazwa kupitia mitandao ya kijamii ukieleza kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amemthibitisha Kaimu Mkurugenzi wa Mwasiliano ya Rais Ikulu Bw. Gerson Msigwa katika cheo hicho na kwamba amemteua Bw. Jerry Murro kuwa Msaidizi wa Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu.


Ujumbe huo wenye kichwa cha habari kilichoandikwa "BREAKING NEWS" unasomeka hivi, nanukuu.

"Mhe Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania amemthibitisha Ndg Geryson Msigwa kuwa mkurugenzi wa mawasiliano Ikulu huku msaidizi wake akiwa ni aliyekuwa msemaji wa Klabu ya Yanga Ndg Jerry Muro" Mwisho wa kunukuu.

Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais Ikulu inapenda kukanusha taarifa hiyo na kuwataka wananchi kuipuuza.

Ifahamike kuwa uteuzi wowote unaofanywa na Mhe. Rais Magufuli hutangazwa na Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais Ikulu ama kupitia Mamlaka rasmi za serikali. Pia huwekwa katika tovuti rasmi ya Ikulu ambayo ni www.ikulu.go.tz

Kwa sasa Mhe. Rais John Pombe Magufuli hajafanya uthibitisho wa Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu Bw. Gerson Msigwa na wala hajamteua Bw. Jerry Cornel Murro kuwa Msaidizi wa Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu kama ilivyoenezwa. Pia hana mpango wa kufanya uteuzi huo.

Ikulu inawaomba wananchi wote kuzipuuza taarifa hizo na kuendelea na shughuli zenu za kila siku. Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu Bw. Gerson Msigwa ataendelea kuwapa taarifa kutoka Ikulu kupitia utaratibu rasmi ambao umekuwa ukitumika.

Gerson Msigwa
Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano, IKULU
Dar es salaam
17 Julai, 2016

No comments:

Post a Comment