Thursday 17 November 2016

Hans Poppe atoa kauli hii kuhusu Simba na Zimbwe JR.

Image result for Hans Poppe
Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Simba, Zacharia Hans Poppe amesema tayari walishamalizana na wachezaji ambao wamekuwa wakizungumzwa kuhamia Yanga.

Kiungo Jonas Mkude na beki Hussein Zimbwe Jr, ni kati ya wachezaji wamekuwa wakihusishwa na kujiunga na Yanga.

Hans Hoppe amesema Simba inajua inachokifanya ni kumalizia vitu vichache tu na wachezaji hao.

“Kila kitu tulishazungumza na kumalizana, kuna mambo madogomadogo sana yanatakiwa kumaliziwa,” alisema Hans Poppe.

“Sasa hao wanaosema maneno mengi, sisi tunaendelea na mambo yetu na si kusikiliza wanasema nini."

Taarifa nyingine zinaeleza, uongozi wa Simba kupitia Hans Poppe umeanza kukutana na wachezaji hao.


USISAHAU KULIKE NA KU-SHARE NA KU-LIKE PAGE YETU FACEBOOK TIKISA MEDIA KUFOLLOW TWITTER @TIKISA MEDIA NA INSTAGRAM TIKISA ENTERTAINMENT MEDIA ILI HABARI ZOTE KUBWA ZIKUFIKIE HAPO ULIPO.ASANTE

                              SUBSCRIBE ON YOUTUBE TIKISA TV

No comments:

Post a Comment