Friday 11 November 2016

PICHA:Tazama jinsi ilivyokuwa wakati wa kuagwa mwili wa Marehemu Samuel Sitta hii leo.



Mwili wa aliyekuwa spika wa bunge la Tanzania, Samuel Sitta umeagwa katika viwanja vya Karimjee na mamia ya watanzania wakiongozwa na Rais wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli na Makamu wa Rais mama Samia Suluhu.


 Wengine ni Rais mstaafu wa awamu ya nne, Jakaya Kikwete, Dk. Gharib Bilal.Baada ya kuagwa Dar, mwili wake utapelekewa Dodoma kwa ajili ya wabunge kutoa saamu za mwisho kisha kupelekwa Urambo, Tabora.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu  Hassan akimpokea mjane wa Spika Mstaafu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Waziri Mwandamizi Mstafu Marehemu Samuel Sitta, Mama Margaret Sitta (kushoto) mara baada ya kuwasili kwenye uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwaongoza viongozi mbali mbali wakati wa mapokezi ya mwili wa Spika Mstaafu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Waziri Mwandamizi Mstafu Marehemu Samuel Sitta

Advertisement


USISAHAU KULIKE NA KU-SHARE NA KU-LIKE PAGE YETU FACEBOOK TIKISA MEDIA KUFOLLOW TWITTER @TIKISA MEDIA NA INSTAGRAM TIKISA ENTERTAINMENT MEDIA ILI HABARI ZOTE KUBWA ZIKUFIKIE HAPO ULIPO.ASANTE

                              SUBSCRIBE ON YOUTUBE TIKISA TV

No comments:

Post a Comment