Tuesday 4 July 2017

Muzamiru Yasin nyota wa simba awa dhahabu Afrika Kusini.

Image result for Muzamiru Yasin
Kiungo nyota wa Simba, Muzamiru Yasin amegeuka lulu kwa baadhi ya timu za Afrika Kusini.

Muzamiru yuko Afrika Kusini akiitumikia timu ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars katika michuano ya Cosafa ambayo imetinga nusu fainali kwa kuwatwanga wenyeji Afrika Kusini.

Taarifa zinaeleza, mawakala kadhaa wameanza kumfuatilia kwa karibu baada ya kuwa mmoja wa wachezaji waliofanya vizuri zaidi.

Moja ya magazeti ya Afrika Kusini yameeleza kuwa Muzamiru ni lulu kutokana na uwezo aliouinyesha katika mechi zote hadi taifa Stars inafikia nusu fainali ya michuano ya Cosafa.


Imeelezwa moja ya timu zilizovutiwa ni Bidvest na Mpumalanga Black Ace lakini wataalamu wanaofuatilia wachezaji au mawakala wanaweza kuwapeleka wachezaji katika timu hata za nje ya Afrika Kusini.

Katika michuano hiyo Muzamiru amekuwa injini kuu ya kuendesha kiungo cha Stars na kusababisha mvuto huo.

No comments:

Post a Comment