Thursday 27 July 2017

Yusuf Manji apeleka ombi Mahakama Kuu.

Image result for manji akiwa mahakamani
Mahakama Kuu ya Tanzania imesema inatarajia kuanza kusikiliza maombi ya dhamana yaliyotolewa na Mfanyabiashara maarufu Tanzania Yusuf Manji, August 4, 2017.

Jaji Isaya Arufani amesema hayo jana baada ya Mawakili wa Serikali Paul Kadushi na Simon Wankyo kuyapokea maombi hayo na kusema wana nia ya kuyapinga huku Jaji akisema anakubaliana na hoja zao na August 4, 2017 maombi hayo ya dhamana yataanza kusikilizwa.

Katika maombi hayo Yusuf Manji anaiomba Mahakama Kuu itengue hati ya kunyimwa dhamana iliyowasilishwa na Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) kwa kuwa ana matatizo ya kiafya akisumbuliwa na matatizo ya moyo.

No comments:

Post a Comment