Tuesday 15 August 2017

Haji Manara aitangaza siku ya semina kwa wanachama wa Simba.

Image result for haji manara

Klabu ya Simba kesho inatarajiwa kufanya Semina kubwa ya Wanachama wote wa klabu hiyo. 

Semina hiyo inalenga kujenga uelewa mpana zaid juu ya muundo mpya wa klabu, uliotokana na mabadiliko ya katiba yaliyofanywa na wanachama hao,na kusajiliwa na Msajili wa Vilabu nchini. 

Maandalizi yote ya Semina hiyo yamekamilika,na itafanyika kesho tarehe 16-8-2017,Jumatano Saa Nane na Nusu mchana(8.30) na itafanyikia kwenye ukumbi wa Mikumi uliopo kwenye eneo la maonyesho ya kimataifa ya biashara ya Sabasaba (PTA) kurasini hapa jijini Dar es salaam. 

Tunawaomba wanachama wote popote walipo waje kwa wingi hapo kesho, huku klabu ikiwaomba viongozi wa Simba Wilaya ya Temeke waandae utaratibu mzuri wa kuwapokea wageni. 

IMETOLEWA NA.... 

HAJI S MANARA

MKUU WA HABARI SIMBA SC 

SIMBA NGUVU MOJA

15.8.2017

No comments:

Post a Comment