Sunday 20 August 2017

Vitu (10) muhimu sana kwa mwanamke kufahamu pindi anapokwenda nyumbani kwa mpenzi wake.

Image result for woman at home activities

1.Ukiingia  nyumbani  kwake ukaona anampigia simu yule dada wa usafi anaye kujaga mara moja kwa wiki aje kufanya usafi alipwe usidhani eti anakujali kiivyo laasha hana kutesiti tu aone kama utasema "acha baby nitakufuria tu ucjali mpenz wangu. Uvivu na kujali


2.Ukikuta kwake amefanya shopping ya vyakula vya kupika kama mchele, unga, maharage, samaki, mafuta na vingine kibao tu halafu anakuambia muende mgahawani mkale dinner my friend usizani eti hana pesa nyingi sana za kutumia."Anakutesti aone kama utamwambia mbaki kwake mpike mle. Fahamu Uko chumba cha mtihani ujue.

3.Ukimtembelea kwake ukamkuta anapika au anafanya usafi halafu wewe unaenda kukaa unaanza kuagalia movie halafu ukitaka kumsaidia anakuambia endelea tu baby kuangalia movie usijali karibu namaliza ,eti na wewe unarudi kwenye kochi miguu juu kwenye sofa unaendelea na movie yako.. "Siku zako zinahesabika

4.Ulishawai kumwambia mpenzi wako aende kwenye ibada ? Alipo kataa ulimsisitiza "Ndugu yangu  hata walevi wanapenda wanawake wanao wasisitiza kwenda kumuomba mungu. "Nikamtihani anakupa.

5.Mara ngapi huwa unamkumbusha kuwaombea dua wazazi wake kama wapo hai au hata kama wametangulia mbele ya haki  AU kumkumbusha kuwajulia hali wazazi wake pamoja na kuwatumia pesa za matumizi "Huo ni mtihani mwingine wakuwa nao makini

6.Jifunze pia kujisiri mwili wako usipende kuacha mwili wako wazi kila wakati hasa ukiwa matembezini au kwenye shughuli zako na pia ukiwa kwake pendelea kukaa karibu yake uwe una mbusu kila atakapo ongea neno nzuri la kufurahisha.

7.Jaribu ukiwa unaenda kwake nenda na tuvitu vitu kama nyanya, vitunguu, na mafuta hivyo vyote wanaume ni shida sana kununua.

8.Wakati mwingine nenda kwake na CD za dini au hata flash yako unaweka mawaidha yanayo mzungumzia Mungu msikilize wote sio wewe kila ukifika kwake wewe ni movie kwenda mbele na music tu sijui wa kina  Diamond, jux na Vanessa ukiwa wa hivyo hata hona tofauti yako na wale macho juu juu anao kutana nao club.

9]Jaribu kumshauri kuhusu kufanya biashara zaidi ya moja yani kuwekeza zaidi , lakini hata kuanzia kufikiria kuhusu kesho kwa mfano ukamwambia unaonaje mpenzi wangu ununue shamba au kiwanja. Wanaume wengi wanapenda mwanamke anaye waza mbali na kufikiri zaidi nje ya Box.


10.Tengeneza utaratibu wako na yeye kwa kuwatembelea watoto yatima na kuwasaidia wahitaji tofauti katika jamii.

No comments:

Post a Comment