Thursday 19 October 2017

Antonio Conte amgeukia na Jose Mourinho juu ya maneno yake ya vijembe.

Image result for conte with jose mourinho
Mkufunzi wa Chelsea Antonio Conte anasema kuwa mkufunzi mwenza katika klabu ya Manchester United Jose Mourinho anafaa kujitazama badala ya kuijadili Chelsea

Conte ameonyesha wasiwasi mkubwa kuhusu kikosi chake cha Chelsea kufuatia misururu ya majeraha msimu huu na kusema kuwa sare ya 3-3 dhidi ya Roma katika michuano ya vilabu bingwa imekifanya kikosi chake kuwa katika hali ya dharura.
Gary Cahill and Marcos Alonso celebrate with Hazard, who scored a brace despite Roma dominating the ball on Wednesday
Mourinho ambaye amewahi kuifunza Chelsea mara mbili alinukuliwa akisema kuwa kuna wakufunzi wengine ambao hupenda kulalama sana kuhusu majeraha.
''Kila wakati Mourinho lazima azungumzie kile kinachoendelea Chelsea," alisema Conte
Alipoulizwa kuhusu matamshi ya Mourinho ambayo hayakumlenga Conte moja kwa moja , kocha huyo wa Itali aliongezea: Kila mara , pia msimu uliopita, nadhani ni wakati anafaa kuzungumzia kuhusu kikosi chake na ajitazame badala ya kutazama wenzake.

No comments:

Post a Comment