Tuesday 24 October 2017

Cristiano Ronaldo anyakua Tuzo ya mchezaji bora kidunia 2017.

He was presented with the award in London by (left to right) FIFA president Gianni Infantino, Diego Maradona and Ronaldo
Cristiano Ronaldo ameshinda taji la shirikisho la soka duniani FIFA la mchezaji bora wa kiume wa kandanda mwaka huu kwa mara ya pili mtawalia.

Tuzo hiyo kwa mchezaji bora mwanamke aliinyakuwa mchezaji wa Uholanzi Lieke Martens, anayeichezea Barcelona.
Mchezaji huyo kutoka Ureno, amefunga mabao 44 katika mechi 48 alizoshiriki katika mwaka, kuiwakilisha nchi yake pamoja na timu anayoichezea ya Real Madrid aliyochangia kufanikisha ushindi wake katika mataji ya ligi ya Uhispania La Liga na Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya.
Barcelona star Lionel Messi arrived with his wife but he failed to pick up the FIFA men's player of the year crown in London
Aliwashinda Lionel Messi wa Barcelona na mchezaji ghali zaidi duniani anayechezea Paris St-Germain, Mbrazil Neymar.
Neymar, the final man up for the player of the year crown, donned a claret jacket at the high-profile event in the English capital

Messi alimpigia kura mwenzake wa Barcelona Luis Suarez naye Ronaldo alimpigia mwenzake wa Real - Luka Modric.
Meneja wa England Gareth Southgate alimpigia kura Ronaldo.

Ufanisi kwa Cristiano Ronaldo

Ulikuwa ni mwaka mwingine wa ufanisi kwa Ronaldo, aliyekuwa ameshinda tuzo ya kwanza ya Mchezaji Bora wa Fifa kwa mwaka 2016.
Aliendeleza ufanisi wake kutoka mwaka uliopita alipowaongoza Ureno kushinda Euro.
Mwaka huu, alifunga mabao mawili katika fainali ya Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya dhidi ya Juventus ambapo walishinda 4-1.
Alifungia klabu hiyo mabao 25 katika mechi 29 alizowachezea na klabu yake ilifanikiwa kushinda La Liga kwa mara ya kwanza katika kipindi cha miaka mitano.
"Tumefika England kwa mara ya kwanza, na nashinda tuzo hii kwa mara ya pili mtawalia. Huu ni wakati mzuri sana kwangu," Ronaldo alisema wakati wa sherehe za kutangaza washindi London Palladium.
Wachezaji watatu bora
Cristiano Ronaldo 43.16 %Lionel Messi - 19.25 %Neymar - 6.97%

No comments:

Post a Comment