Tuesday 31 October 2017

Ndugai:kitendo alichokifanya Lazaro Nyalandu ni umbea.

Image result for spika job ndugai
SPIKA wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Job Ndugai, amesema kwamba hana taarifa za kujiuzulu kwa mbunge wa Singida Kaskazini Lazaro Nyalandu na wala hiyo barua bado haijamfikia, amekiita kitendo alichokifanya ni umbea.


Job Ndugai ameyasema hayo leo alipokuwa akizungumza na chombo kimoja cha habari nchini (jina tunalo) na kusema kwamba Lazaro hakupaswa kutangaza hivyo kabla ya kuhakikisha barua imemfikia.

Pamoja na hayo Spika Ndugai amewataka wabunge wengine kuacha kuwashwa washwa na kufanya mambo ambayo ameyaita ni ya umbea.

No comments:

Post a Comment