Monday 16 October 2017

Rais Magufuli amtumbua mwenyekiti wa bodi ya Kilimanjaro Airports Development Company

Image result for Balozi Hassan Gumbo
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli leo Oktoba 16, 2017 ametengua uteuzi wa Mwenyekiti wa bodi ya Kilimanjaro Airports Development Company (KADCO), Balozi Hassan Gumbo.


Kwa taarifa iliyotolewa leo na Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Dkt. Leonard Chamuriho imesema kuwa Rais Magufuli amemteua Gregory George Teu kuwa Mwenyekiti mpya wa Bodi ya Kilimanjaro Airports Development Company (KADCO).
Mbali na hilo Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Prof. Makame Mbarawa naye ametengua uteuzi wa mjumbe wa bodi hiyo Bw. Suleiman Suleiman kuanzia leo. 

No comments:

Post a Comment