Tuesday 24 October 2017

VIDEO:Lifahamu Goli Bora lililompa Tuzo ya dunia Olivier Giroud.

Arsenal striker Olivier Giroud won the FIFA Puskas award for the best goal of the year
Bao alilolifunga mchezaji wa klabu ya Arsenal ya Uingereza Olivier Giroud dhidi ya Crystal Palace limeshinda tuzo ya Bao Bora la Fifa mwaka 2017, maarufu kama Tuzo ya Puskas.

Alifunga bao hilo siku ya Mwaka Mpya katika Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya.
Kwenye bao hilo maarufu kama 'scorpion kick', Giroud aliufikia mpira kutoka kwa mshambuliaji Alexis Sanchez kutoka nyuma yake akaupiga kwa mguu wake wa kushoto na kuupitishia juu ya bega kisha ukaugonga mwamba wa goli kabla ya kutulia kimiani.
Giroud scored a stunning scorpion kick against Crystal Palace in the Premier League
Bao hilo la Giroud lilipata kura 36.1% kati ya jumla ya kura 792,062 zilizopigwa.
Giroud alikuwa anashindania tuzo hiyo na Deyna Castellanos wa Venezuela na kipa wa Afrika Kusini Oscarine Masuluke.

No comments:

Post a Comment