Real Madrid wanalenga kumsajili beki
wa Chelsea na Brazil David Luiz 30 ambaye hatakikani katika uwanja wa
Stamford Bridge msimu huu. (Daily Mail)
Mkufunzi wa Chelsea
Antonio Conte anasema kuwa hajaelezwa iwapo atalazimika kuwasajili
wachezaji wowote katika dirisha la uhamisho la mwezi Januari iwapo
mabingwa hao watetezi wanatarajiwa kuwafikia viongozi wa ligi Manchester
City. (Guardian)
Mchezaji wa Manchester City na raia wa Ujerumani
mwenye umri wa 21 Leroy Sane atapewa kandarasi mpya na Manchester City
mwishoni mwa msimu huu. (Sun)
Watford wameonya kwamba mshambuliaji
wao raia wa Brazil Richarlison, 20, ambaye alijiunga na klabu hiyo kwa
mkataba wa miaka mitano kutoka Fluminence mnamo mwezi Agosti kwa kitita
cha £11m na anavutia klabu za Tottenham na Chelsea hauzwi wakati wa
dirisha la uhamisho la mwezi Januari. (London Evening Standard)
Chelsea wanatarajiwa kumnunua beki wa Juventus Alex
Sandro ,26, mwezi Januari baada ya kushindwa kumsajili mshambuliaji huyo
wa Brazil mwaka uliopita.(Daily Express)
Liverpool na Leicester
wanaangazia kumsajili beki wa West Brom na Misri Ahmed Hegazi, 26,
ambaye yuko katika mkopo kutoka klabu ya Al Ahly. (ESPN)
Kiungo wa kati wa Manchester City David Silva, 31,
anatarajiwa kuandikisha mkataba mpya ambao utamweka mchezaji huyo wa
Uhispania katika uwanja wa Etihad hadi 2020. (Daily Mirror)
City
haitamuuza mlinzi wa Ufaransa Eliaquim Mangala mnamo mwezi Januari ,
lakini mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 26 hajapewa thibitisho kuhusu
hatma yake katika klabu hiyo. (Goal)
Liverpool na Juventus wote
wanataka kumsajili winga wa klabu ya Sporting Lisbon mwenye umri wa
miaka 22 raia wa Ureno Gelson Martins. (A Bola, via Talksport)
Mkufunzi wa Arsenal Arsene Wenger anasema kuwa afisa
mkuu mtendaji wa klabu hiyo Ivan Gazidis hausiki na mpango wa
kuwanunua wachezaji kufuatia mabadiliko yaliofanyika katika klabu
hiyo(Daily Mail)
Mchezaji anayesakwa na klabu ya Manchester City
na Napoli Sime Vrsaljko anataka kuondoka Atletico Madrid. Beki hiyo huyo
mwenye umri wa miaka 25 raia wa Croatia anatafuta changamoto
mpya(Talksport)
Mshambuliaji wa Atletico Antoine Griezmann
angejiunga na Arsenal mwaka 2013 lakini the Gunners wakaamua kutomsajili
mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 26 na wakati waliporudi kutaka
kumsajili alikataa (Daily Express)
Swansea inapigiwa upatu kumsajili mshambuliaji wa Liverpool Dominic Solanke, 20. (Wales Online)
Beki
wa Arsenal na Ufaransa Laurent Koscielny, 32, anataka kumaliza mchezo
wake katika klabu ya Lorient, kulingana na rais wa klabu hiyo ya
Ufaransa (Canal+, via Goal)
Arsenal ni miongoni mwa vilabu kadhaa
vya ligi ya Uingereza wanaotaka kumsajili Novara Calcio mwenye umri wa
20 raia wa Uholanzi Alessio da Cruz. (Daily Mirror)
Mshambuliaji wa Liverpool Divock Origi, ambaye yuko
Wolfsburg kwa mkopo hajui hatma yake katika klabu ya Anfield, huku
mchezaji huyo wa Ubelgiji akiendelea kuvutia katika ligi ya Ujerumani ya
Bundesliga. (Liverpool Echo)
Mshambuliaji wa Newcastle Alex
Gilliead mwenye urmi wa miaka 21 ambaye yuko kwa mkopo katika klabu ya
Bradford, anatakiwa na klabu ya Hull, Millwall na wapinzani wao
Sunderland. (Newcastle Chronicle)
No comments:
Post a Comment