Tuesday 28 November 2017

Yanga yatoa mapumziko kwa wachezaji wake.



Baada ya ligi kusimama kwa muda wa wiki moja, kikosi cha Yanga sasa kitakuwa na mapumziko ya siku kadhaa.

Ruhusa hiyo imetolewa na Kocha Mkuu wa Yanga, George Lwandamina ambaye amewapa wiki  moja wachezaji wake kupumzika.

Kikosi cha Yanga kipo mapumziko baada ya kucheza mechi 11 na kikishika nafasi ya tatu nyuma ya Simba na Azam katika Ligi Kuu Bara huku mchezo wa mwisho timu hiyo ikiwa imecheza dhidi ya Tanzania Prisons na mchezo kumalizika kwa sare ya bao 1-1.

Yanga ina pointi 21, ikizidiwa pointi mbili mbili na Simba, sawa na Azam FC ambayo jana ilitoka sare ya bao 1-1 dhidi ya Mtibwa Sugar kwenye Uwanja wa Azam Complex.


No comments:

Post a Comment