Saturday 20 January 2018

Donald Ngoma atinga mazoezini Yanga kwa mtindo huu.


Mshambuliaji wa Yanga, Donald Ngoma bado ni majeruhi na hajajiunga na wenzake.

Lakini jana aliamua kuwatembelea wenzake mazoezini kwenye Uwanja wa Uhuru wakati wakiendelea kujifua kujiandaa na mechi za Ligi Kuu Bara.


Raia huyo wa Zimbabwe, ameendelea kukaa nje kwa zaidi ya miezi miwili sasa na imekuwa zaidi ya wiki tatu tokea arejee Dar es Salaam akitokea kwao Zimbabwe ambako ilielezwa amekwenda kupata matibabu nchini Afrika Kusini.

No comments:

Post a Comment